wito kwa filamu za muziki

 

call for music filmswito kwa filamu za muzikiappel aux Films
 
Film page banner

Mpango wa filamu za muziki wa kiafrika wa siku nne katika tamasha la Sauti za Busara huonesha filamu za muziki ndefu na fupi pamoja na video kama kiongezeo cha show za live za wasanii kwenye jukwaa juu, Mara iliyopita sehemu ya kukaa ya amphitheatre ilibadilishwa kuwa nafasi kwa ajili ya sinema ya muziki wa kiafrika ambapo washabiki na wapenda tamasha hukusanyika pamoja kuangalia filamu saba za kiafrika kuona filamu nyingi zinavyo kusanywa kutoka afrika.

Ni nini tunatafuta...

Sauti za Busara inatafuta filamu ndefu pamoja na filamu fupi fupi zenye kusisimua kutoka bara la afrika, ambazo zitakuwa zikionyeshwa kuanzia saa moja wakati wa tamasha mwezi wa pili. Filamu hizi ziwe kivutio na kiburudisho katika bara la Afrika. Hii inaweza kuwa ni ala za muziki na video, burudani zilizonakiliwa, kimsingi tunatafuta:

  • Filamu za muziki ambazo zina ujumbe wa muziki wa bara la Afrika na mabara yanayohusiana na Afrika.
  • Filamu za muziki ambazo ni za kipekee na zitakazowavutia watazamaji wote( kitaifa na kimataifa n.k)
  • Filamu za muziki zinazowakilisha aina ya utajiri wa muziki kutoka Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.
  • Filamu za muziki zenye ubora na maadili ya kiafrika.
  • Filamu za muziki ambazo zinaujumbe mpya na ambao haujawahi kusikika pamoja na wasanii wapya.
  • Filamu za lugha za kigeni ambazo zina mfumo wa Kiswahili au kiingereza

Mwisho wa kutuma maombi ni: 30 September 2011
Maombi yako yatashughulikiwa ikiwa tutapokea maombi pamoja na kopi mbili za filamu yako kabla ya tarehe 30 September 2011. Waombaji wote watajulishwa maamuzi ya jopo la uchaguzi ifikapo mwezi November.

Jinsi ya kutuma maombi ni rahisi...

Hatua ya kwanza :
Jaza:fomu hii ya maombi.

Hatua ya pili:
*Njia ya kutufikia mpaka mlangoni
Ofisi ya Busara Promotions, Tumetizamana na Golf Club, Maisara, Njia iendayo uwanja wa ndege, Zanzibar, Tanzania
*kwa njia ya posta
Busara Promotions, PO Box 3635, Stone Town, Zanzibar, Tanzania

Hatua ya tatu:
Tuma picha au filamu zenye ubora kupitia barua pepe ifuatayo busara@busara.or.tz