Habari za tamasha la Sauti za Busara 2012 | Picha za 2012 | English version
|
||||
Muziki wa Afrika – chini ya mawingu ya Afrika. Sauti za Busara ni tamasha linalo fanyika kila mwaka hapa Afrika ya mashariki na limekuwa lijulikana kama “Tamasha rafiki zaidi duniani”. Tamasha la nane la Sauti za Busara litafanyika tarehe 8 mpaka 12 Februari 2012. Likija pamoja na
Wanamuziki 400 : Hivyo ni vikundi arobaini, ishirini vikitoka hapa hapa Tanzania, na ishirini kutoka sehemu nyingine za Afrika. Vikundi vya mijini, mashamba, vikundi vinavyotumia vyombo vya umeme, vilivyoanzishwa na vikundi chipukizi.
Siku nne ndani ya Ngome Kongwe: Ndani ya mji mkongwe, Alhamis mpaka Jumapili na muziki usioisha wa "live" (no playback) huendelea kila siku kutoka saa 11 jioni mpaka saa 7 usiku.
Filamu za Muziki wa Kiafrika : Filamu za muziki za kumbukumbu, filamu ndogo ndogo za muziki, video, na filamu za burudani za laivu.
Maandamano: Maandamano ya tapitayo barabara kuu katika siku ya pili, ikiwemo ngoma ya beni, ngoma za kienyeji, kikundi cha wanawake cha mwanandege, sarakasi, na viburudisho vingi vya kushangaza. Angalia Maandamano ya Ufunguzi.
Semina za Mafunzo: Kuwajenga wasanii, viongozi, waandishi wa habari, watengeneza filamu, na mafundi wa vipaza sauti na taa kuwa na ujuzi endelevu kutoka hapa Afrika ya mashariki.
Waanzilishi wa Sanaa: Makongamano ya kila siku yanayowakutanisha wataalamu wa sanaa wa hapa nyambani na wakigeni.
Tamasha na soko: vyakula vya kienyeji na vinywaji, muziki,mapambo, mavazi, na vitu vilivyotengenezwa kwa mikono.
Busara Xtra: Wakati wa tamasha Kisiwa cha Zanzibar hurindima na matukio tofauti. Ngoma za kienyeji, ngoma za kudensi, shoo za kiana, mashindano ya ngalawa, viburudisho vya baada ya pati, na burudani za taarabu asilia hupangwa na wenyeji.

"Tamasha la Sauti za Busara huwavutia vijana wa kizanzibar na kuwaleta pamoja na utamaduni wao, kutoa nafasi kwa wasanii na wataalamu wa muziki kukutana na kujifunza kutoka kwa kila mmoja. Kuuweka utamaduni hai, kutoa ajira kwa wenyeji, na kuikuza Zanzibar kama mfano katika sekta ya utalii-inayoheshimu utamaduni wa kizanzibar."
Yusuf Mahmoud, Festival Director