Sauti za Busara 2007 |
top |
Tamasha la nne la Sauti za Busara litafanyika kama kawaida mwezi wa Februari, kuanzia tarehe 9 hadi 14 2007; na kama kawaida kiingilio ni bure kabla ya saa mbili usiku kila siku.
|
|
Tamasha hili hufanyika kila mwaka katika kipindi ya katikati ya mwezi wa Februari,na ni tukioi ambalo huvutia watu wa jinsia , rika, Imani na mataifa mbalimbali katika kujionea na kusherehekea utajiri wa aina mbalimbali za muziki wa waswahili na watu wa Afrika ya Mashariki. Tamasha hili huonyesha aina mbalimbali za muziki na maonyesho ya jukwaani
hususan kutokea Afrika ya Mashariki, pamoja na baadhi ya vikundi kutoka
nje ya Afrika Mashariki hualikwa pia. Mwaka huu tamasha litafanyika katika
uwanja wa Ngome Kongwe eneo la Mji Mkongwe, vile vile maonyesho mengine
yanatarajiwa kufanyika katika vitongoji mbalimbali pembezoni mwa Mji Mkongwe,
na mojawapo ya fukwe maridadi Zanzibar. |
Zaidi ya vikundi na wasanii mia moja wameshiriki katika moja ya matamasha yaliyopita ya Sauti za Busara na baadhi yao ni Juma Nature & Wanaume family, Saida Karoli, Mchinga Generation, Ferooz na Das Nundaz, Eric Wainaina ( Kenya), Ghorwane ( Mozambique), The Shrine Synchrosystem ( Uingereza), Taffetas ( Uswisi), Atongo Zimba ( Ghana), African Revolution Band, Maulid ya Hom, El Tanbura ( Misri), Seiyun Popular Arts ( Yemen), Culture Music Club, Chibite, Wagosi wa Kaya na wengineo wengi.
Baadhi ya wasanii wa Afrika ya Mashariki kama Afrikali Band, Oya Theatre, Zemkala, Jagwa music, X Plastaz, Sina Chuki Kidumbak na wengineo wameanza kupata mialiko ya kushiriki matamasha nje ya nchi baada ya kuonekana katika tamasha la Sauti za Busara.
Je unataka kushiriki?
Kwa wasanii wanaotaka kushiriki katika tamasha lijalo la 2007, unatakiwa kutuma maombi yako kabla ya mwisho wa mwezi wa Agosti. Tuma maombi yako kwa njia ya barua pepe (email) au barua ya kawaida kwa ofisi ya Busara Promotions (Anuani hapo chini). Maombi yaambatane na nakala za kazi yako ya hivi Karibuni (CD, Kanda za kaseti na/au video). Picha pamoja na maelezo ya kina ya msanii au kikundi, na pia kama una kumbukumbu za maelezo kutoka katika vyombo vya habari juu yako tafadhali ambatanisha pia.
Kwa wasanii wanaochaguliwa kushiriki katika tamasha la Sauti za Busara, gharama
zao za usafiri, malazi, chakula na malipo ya onyesho zitalipwa na waandaaji
(Busara Promotions). Wasanii kutoka nje ya Afrika Mashariki watatakiwa kujilipia
wenyewe gharama za usafiri.
Tamasha hili lisingeweza kuwa lenye mafanikio kama si kwa mchango mkubwa wa wadhamini na wafadhili mbalimbali.
Busara Promotions imeandaa taarifa maalum kwa wadhamini na wafadhili mbalimbali juu ya namna ya kushirikiana ili kufanikisha tamasha la nne la Sauti za Busara. Taarifa hiyo imeambatanishwa na DVD ya tamasha, azimio, bajeti na orodha ya namna mbalimbali ambazo jina lako linaweza kuwa miongoni mwa wafanikishaji wake. Iwapo una nia ya kushirikiana nasi tafadhali wasiliana nasi.
Kama unayo nafasi ya kulitangaza tamasha la Sauti za Busara tunatanguliza shukrani za dhati kwa msaada wako.
Je unayo orodha ya anuani za barua pepe, tovuti, ubao wa matangazo au nafasi katika jarida?
Maneno machache tu na taarifa juu ya tovuti yetu yatasaidia sana. Nasi pia tutakuwa tayari kukutangaza katika moja ya kurasa za tovuti yetu.
Tunaweza pia kukutumia matangazo ya ukutani (posters) na postikadi za tamasha kama si gharama sana.
Si filamu kamili, lakini kuna filamu kibao fupi, picha na maelezo ya tamasha katika tovuti mbalimbali:
| Filamu fupi za tamasha la mwaka 2006 |
|
| Taarifa mbalimbali za tamasha la mwaka 2006 |
|
| Taarifa mbalimbali za tamasha la mwaka 2005 |
|
| Taarifa mbalimbali za tamsha la mwaka 2004 |
|
| Taarifa mbalimbali za tamasha la mwaka 2006 |
Wasanii wetu |
top |
Mshindi
wa tuzo ya WOMEX 2005, Bi Kidude atakuwa tena ziarani barani Ulaya wiki hii,
akiambatana na kundi lake la Unyago. Msanii huyu mkongwe lakini ambaye anendelea
kutamba katika ulimwengu wa sanaa, atafanya maonyesho matatu katika tamasha
la kimataifa lijulikanalo kama Festival
Mundial nchini Uholanzi kati ya terehe 15 na 18. Vile vile Bi Kidude atapata
nafasi ya kuzungumzia filamu yake inayotarajiwa kuzinduliwa hapo mwezi wa Februari
2007 ijulikanayo kama “As Old As My Tongue” inayotengenezwa na kampuni
ya ScreenStation
UK.
Upigaji picha za filamu hii ulianza miaka mitatu iliyopita hapa Zanzibar na katika safari mbalimbali za kimuziki za Bi Kidude. Zaidi ya kuwa ni filamu inayoelezea maisha yake, inaelezea mambo mbalimbali ya kisiasa, kiutamaduni na kijamii kisiwani Zanzibar.
Bi Kidude ni msanii ambaye anafahamika kama shujaa aliyepamabana na vikwazo vingi hadi kufikia hapo alipo. Na amejijengea himaya ya mashabiki wengi ndani na nje ya nchi. Yeye ni kipenzi cha Masultani, Marais na mabaharia wa kale wa majahazi, historia yake ni changamoto kuwa umri si kikwazo cha kutimiza ndoto zetu. Bi Kidude hupendelea kukaa nyumbani kwake akiwa na wajukuu, jamaa na marafiki, yeye ni mwongeaji sana na mpenda wageni, pia hupendelea kuvuta sigara.
Umewahi kusikia
kuhusu Bongo Flava na Congotronics. Kaa tayari sasa kwani
“Bongotronics” inakuja, ni muziki wenye umaarufu katika maeneo ya watu
wa kipato cha chini jijini Dar es Salaam.
Jagwa Music ni kikundi kinachopiga muziki wa mchiriku ambao ulizaliwa kutoka katika muziki wa kimwambao ujulikanao kama chakacha. Ala zinazotumika katika muziki huu ni pamoja na Keyboard ndogo ya mkono, ngoma, filimbi, mkwasa, kibao cha kukalia na wakati mwingine gitaa pia hutumika.
Mwaka 2005 Jagwa Music ilipata nafasi ya kwenda nchini Uingereza kushiriki katika tamasha la WOMEX, na waliweza kuwa kivutio kikubwa hasa kutokana na uchezaji wake. Na tayari waandaji wa matamasha kutoka nchi mbalimbali wameanza kutoa mialiko kwa kikundi hiki.
Jagwa wamerekodi albamu zaidi ya kumi katika kanda za kaseti, lakini kwa mara ya kwanza mwaka huu wameweza kurekodi CD yao ya kwanza ambayo inafanyiwa marekebisho nchini Ujerumani na itazinduliwa mapema mwaka 2007.
Vilevile kwa mara ya kwanza wamerekodi kanda ya video ya kwanza inayojulikana kama Maisha Popote, na inatarajiwa kurushwa katika vituo mbalimbali vya televisheni hivi Karibuni.
Yajayo |
top |
Tamasha la Nchi za Jahazi – ZIFF
|
Tamasha la Avante Mozambique!
|
Nafasi |
top |
Busara
Promotions inatafuta mtu atakayeweza kufanya kazi na kupata mafunzo ya kuwa
msimamizi wa shughuli za sanaa kwa kipindi cha kuanzia mwezi wa Agosti 2006
hadi Machi 2007.
Mwombaji ni lazima awe raia wa Afrika Mashariki na mwenye moyo wa kupenda na kutaka kutunza muziki wa kiafrika. Ni muhimu kwa mwombaji kuwa na ujuzi wa msingi wa Kompyuta, ufahamu wa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.
Kwa yule atakayepata nafasi hii atakuwa akipata mafunzo kazini amabayo ni pamoja na masuala ya uandaaji wa matamasha, semina, warsha, namna ya kufanya matangazo, kusimamia wasanii na ufahamu wa sura ya muziki wa Afrika Mashariki.
Atakayechaguliwa katika nafasi hii atafanya kazi katika ofisi za Busara Promotions zilizopo eneo la Mji Mkongwe Zanzibar, na awe tayari kusafiri pale atakapohitajika. Busara Promotions itagharamia posho ya kujikimu na vile vile mwombaji atapata cheti maalum mara tu baada ya kumaliza mafunzo na tunamini ya kuwa nafasi hii itamwezesha mwombaji kuwa dereva bora katika maendeleo ya muziki Afrika Mashariki.
Kwa yeyote atakayependa kuomba nafasi hii basi tafadhali tuma barua
pepe au kwa njia ya posta ikiambatanishwa na vielelezo vya kuthibitisha
uwezo wa mwombaji, ili viweze kufika ofisi za Busara promotions kabla ya tarhe
27 Juni 2006.
Occasionally Busara Promotions is able to offer short term placements for skilled and experienced music professionals, for example: music producers and sound engineers. Such placements are usually on a voluntary basis and involve on-the-job training of Tanzanians.
Contact us for more details in case you fit the bill.
![]() |
|
Tamasha la B-Connected |
top |
Dar es Salaam – 21 Mai 2006
Busara Promotions imefarijika kwa kushirikishwa katika tamasha la B-Connected mbalo liliambatana na matamsha mengine katika nchi za Afrika Kusini, Ethiopia, Hungury na Uholanzi.
“Hili ni tamasha zuri sana kuliko mengine niliwahi kuhudhuria” Joshua kijana wa kimasai aliyekuwa akivuja jasho kutokana na kucheza muziki alimwambia mwandishi wa Daily News
Wengi wa wasanii washiriki walipata nafasi ya baada ya kushinda katika mashindano yaliyoandaliwa kwa ajili ya kusaka vipaji vya wasanii wachanga. Mwanzoni mwa mwezi wa Mei Busara ilishiriki kama mmoja wa majaji wa shindano la kusaka vipaji Zanzibar na pia iligharamia usafiri wa kwenda na kurudi Dar es Salam – Zanzibar kwa washindi ambao walikuwa ni BZ Brook wa upande wa muziki wa kizazi kipya na Shirkisho Sanaa Group kwa ngoma za asili.
Busara Office: CD faves |
top |
Looking for some music suggestions? Here’s what’s getting played in the Busara Office at the moment:
| Toumani Diabate & Symmetric Orchestra |
Boulevard de l’Independence |
(Mali) |
World Circuit |
| Gigi |
Gold & Wax |
(Ethiopia) |
Palmbeat |
| Wanaume Family TMK |
Ndio Zetu |
(Tanzania) |
Bongo Records |
| Ursula Rucker |
Ma’at Mama |
(USA) |
K7 |
| Various Artists |
Midnight in Mali |
(Mali) |
Sterns |
| Tiken Jah Fakoly |
Coup De Gueule |
(Ivory Coast) |
Wrasse |
| Various Artists |
Rough Guide to Tanzania |
(Tanzania) |
World Music Network |
| Gotan Project |
Lunatico |
(France) |
XL |
| Natacha Atlas |
Mish Maoul |
(UK) |
Mantra |
| Samba Mapangala |
Song & Dance |
(DRC) |
Virunga |
| The Streets |
The Hardest Way to Make an Easy Living |
(UK) |
679 |
| Atongo Zimba |
Savannah Breeze |
(Ghana) |
Hippo Records |
Utabiri wa hali ya hewa – Zanzibar – February 2007 |
top |
![]() |
![]() |
![]() |
||
![]() |
![]() |
|
![]() |
Wasiliana Nasi |
top |
![]() |
Busara Promotions, PO Box 3635, Zanzibar, Tanzania +255 24 223 2423 or +255 777 428 478 Find us in Stone Town, between Africa House and Serena Hotel, opposite Amore Mio.
|
| We are continually in the process of revising and updating our mailing-list. If you have received this more than once, or would prefer to receive it at another address, please let us know. Alternatively, you can click here to unsubscribe. |
|