Wito kwa vikundi vyote vya Afrika!
Je muziki wako ni asilimia mia live?
Je muziki wako ni wa kiafrika?
Je unania ya kushiriki katika tamasha lijalo Februari Afrika Mashariki?
Kama jibu ni ndiyo – shiriki sassa kwa kutuma maombi yako tuma sasa !
Tamasha la Sauti za Busara linawajumuisha watu pamoja. Kila februari ndani ya Mji Mkongwe ni muziki live na vionjo vya Afrika. Ni siku tano katika jukwaa hii ikiwa ni vikundi ishirini kutoka Tanzania na ishirini kutoka sehemu zingine barani Afrika. Asilimia mia ni live – si ruhusa kuimba kwa kutumia cd. Mambo mengine yanayofanyika wakati wa tamasha ni maandamano ya ufunguzi, mikutano na mafunzo mbali mbali.
Miaka iliyopita zaidi ya vikundi 280 vilishiriki , ikiwa pamoja na Jose Chameleone, Samba Mapangala & Orchestra Virunga, Didier Awadi, Bassekou Kouyate & Ngoni ba, Thandiswa, Jagwa Music, Ba Cissoko, Nyota Ndogo, Natacha Atlas, Culture Musical Club na wengineo
Ni rahisi kutuma maombi
Kikundi kitashughulikiwa endapo tutapokea fomu
na nakala ya kazi ya msanii kabla ya tarehe 31 July 2010.
Jopo la uchaguzi litakaa na kuchagua vikundi vitakavyoshiriki katika tamasha. Vikundi vyote vitajulishwa ifikapo mwezi wa tisa.
Kwa wasanii watakaochaguliwa kushiriki katika tamasha kwa kawaida waandaji wa tamasha hulipa ada ya onyesho pamoja posho kwa kila msanii awapo Zanzibar,hii ikiwa ni usafiri, malazi, chakula na matumizi madogo.Kwa wasanii kutoka nje ya Tanzania huwa tunawasaidia kutafuta wadhamini wa usafiri.
|