Matona's G Clef Band
Country Zanzibar Genres fusion Website /mohamed.matona Festival Sauti za Busara 2017 Recordings 📼 Urithi 2006
Kikundi cha G Clef au kwa jina jengine kinajulikana kama ‘Kikundi cha Matona’, kilianzishwa mwaka 1995 baada ya kubinafsishwa kwa hoteli ya Bwawani. Matona alikuwa kiongozi wa kikundi kilichojulikana kama Kikundi cha Taarab cha Bwawani, hoteli ilipobinafsishwa kikundi hakikuvunjika, kiliendelea kwa jina jengine ambalo ni G Clef Taarab Orchestra, wanakikundi hawa waliendeleza kupiga muziki wa taarab.Na pale wanamuziki wakongwe walipokuwa wakihama kikundi, Matona alikuwa akileta wanamuziki vijana ambao akiwafundisha ujuzi mwenyewe.Hatimaye kikundi hichi kikawa maarufu Zanzibar. Wakawa manapiga nyimbo tofauti, hata za kihindi, kiarabu, muziki wa dansi na hata muziki wa rock.
Kikundi hichi kilisitisha sanaa kwa muda pale Matona alipojishughulisha na ufunguzi wa shule ya muziki ya DCMA mwaka 2001. Matona alikifufua kikundi hichi mwaka 2015 baada ya kuona kuna nafasi ya kuwepo kikundi cha muziki ambacho kitapiga aina tofauti za muziki. Na sasa ni kikundi kinachojulikana sana mjini. Madhumuni yao ni kuendeleza aina tofauti za miziki inayopigwa katika nchi za afrika ya mashariki kama vile taarab, mgodro, salege, chakacha, sega, na mbiwi.
Algeria Angola Australia Austria Benin Burkina Faso Burundi Cameroon Canada Cape Verde Comoros Congo Côte d'Ivoire Denmark DRC Egypt eSwatini Ethiopia Far East Finland France Gambia Germany Ghana Guinea Guinea Bissau Iraq Japan Kenya Lesotho Madagascar Malawi Mali Mauritania Mauritius Mayotte Morocco Mozambique Namibia Netherlands Nigeria Norway Pan Africa Pemba Puerto Rico Reunion Rwanda Senegal Seychelles Somaliland South Africa Sudan Suriname Sweden Switzerland Tanzania Uganda UK USA Various Yemen Zambia Zanzibar Zimbabwe
acoustic acrobats afrobeat band blues bongo flava coastal comedy dance dj electro fusion hiphop jazz kidumbak pop reggae rock roots rumba spiritual spoken word taarab traditional urban zenji flava