Comrade Fatso & Chabvondoka
Country Zimbabwe Genres band fusion hiphop reggae Website www.comradefatso.com Festival Sauti za Busara 2009, 2013 Recordings 📼 House of Hunger, 2008; Korokoza (single), 2011
Comrade ni mkali wa mashairi kutoka Zimbabwe. Amejifunza mambo mengi ya muziki katika nchi tofauti kama Marekani, Uingereza, Ujerumani na Ufaransa. Maranyingi hujitahidi kuwaburudisha na kuwatolea ujumbe mashabiki wake.
Comrade na bendi yake ni kikosi kazi chenye kutoa radha tofauti za muziki kama Rock, hip hop, chimulenga, jit, kwaito na reggae. Walitoa albamu waliyoipa jina la nyumba ya njaa (House of hunger) lakini bahati mbaya ilipigwa marufuku nchini Zimbabwe kutokana na hali ya kisiasa. Wameshafanya maonyesho ndani ya bara la ulaya, Marekani, Karibiani na Afrika. Mwaka 2010 walifanya onyesho katika tamasha kubwa lijulikanalo Exit Festival.
Comrade alifanya ziara tena katika bara la ulaya mwaka 2011 katika tamasha la Uppsala International Poetry Festival nchini Sweden na ziara ndefu ya mwezi mzima nchini Denmark. Albamu ya hivi karibuni ijulikanayo kama Korokoza imefanikiwa kupata sifa ulimwengu mzima kutokana na maudhui yake na mpangilio wa mashairi ambayo ni adimu katika masikio ya watu wengi.
Algeria Angola Australia Austria Benin Burkina Faso Burundi Cameroon Canada Cape Verde Comoros Congo Côte d'Ivoire Denmark DRC Egypt eSwatini Ethiopia Far East Finland France Gambia Germany Ghana Guinea Guinea Bissau Iraq Japan Kenya Lesotho Madagascar Malawi Mali Mauritania Mauritius Mayotte Morocco Mozambique Namibia Netherlands Nigeria Norway Pan Africa Pemba Puerto Rico Reunion Rwanda Senegal Seychelles Somaliland South Africa Sudan Suriname Sweden Switzerland Tanzania Uganda UK USA Various Yemen Zambia Zanzibar Zimbabwe
acoustic acrobats afrobeat band blues bongo flava coastal comedy dance dj electro fusion hiphop jazz kidumbak pop reggae rock roots rumba spiritual spoken word taarab traditional urban zenji flava